Jinsi ya Kuondoa Sumu Mwilini Milele

Jinsi ya kuondoa sumu mwilini milele

Kwenye somo lililopita tulijifunza sumu mbalimbali zinazoweza kumfanya mtu akawa mnene au akapata shida kupungua.

Ni ukweli kwamba kama kila siku unaingiza kitu kinachokufanya uongezeke, sio rahisi ukapungua.

Na kama tayari mwilini kuna sumu zinazokufanya uendelee kuwa mnene, ni wazo zuri kuondoa kwanza hizo sumu.

Hata hivyo..

Kuna sumu zingine ambazo haziongezi uzito moja kwa moja, ila zinaathiri ini ‘kiungo kikuu cha kuchakata sumu’.

Siku zote, ini pamoja na viungo vingine kama figo huwa vinapambana kuondoa sumu ambazo zinaingia mwilini.

Sumu tunazipata kutoka katika vyanzo mbalimbali, vingine vinaepukika na vingine hatuwezi kuviepuka kama vile uachafuzi wa hali ya hewa.

Kwa vyanzo ambavyo vinaepukika kama dawa na vyakula ni vema kuviepuka kama nilivyofundisha kwenye somo lililopita.

Kwa vyanzo ambavy haviepukiki ni vema kujua njia ambazo zinaondoa sumu kila siku.

Yaani..

Kwa sababu sumu zinaingia mwilini mwako kila siku, ufahamu njia za kuziondoa kila siku bila kuwa kwenye program Fulani hivi maalumu.

Kwanini kila  mtu ni muhimu kufahamu mambo haya?

Tumezungukwa na bahari ya sumu..

Yaani, saiv kila kitu kwa namna moja au nyingine kinaweza kuwa kinaogeza sumu kwenye mwili wako.

Kuanzia kwenye chakula, dawa, vyombo vya kupikia, kulia, hewa tunayovuta, maji ya kunywa, mafuta ya kupaka, perfume, na huko kazini inategemeana unafanya kazi gani kunaweza kukawa na kemkili mbaya ambayo inaweza kuathiri afya yako.

Hakuna mtu ayanaishi mbinguni..

Hata hivyo hizi sumu zinatofuatiana ukali kwa maana ya namna ambavyo zinaathiri mwili kulingana na dozi na aina ya sumu yenyewe.

Kwahiyo..

Kwa zile sumu kali ambazo zinaepukika, fanya jitihada za kuepuka..

Madhara ya kutoondoa sumu

Unapowaza kuhusu madhara ya sumu mwilini, kumbukuka kuwa na kemikali ambazo zinaathiri uwezo wa mwili kufanya kazi sawa sawa.

Kwahiyo inaweza kuathiri mwili mzima katika mifumo mbalimbali, kama;

Magonjwa ya moyo na mishipa ya damu. Zinaweza zisisababishe moja kwa moja lakini zinaweza kuchangia kwenye magonjwa kama presha, kiharusi.

Inachangia kutokea kwa upinzani wa insulin na kupelekea magonjwa kama kisukari. Na mafuta kujazana hasa kwenye tumbo.

Mojawapo ya sababu kwanini wakati mwingine kitambi kianachelewa kuondoka ni kwa sababu ya upinzani wa insulin ambao inachukua muda kuondoka unapokua umeanza program.

.. ukiona unapambana mwezi mzima huoni matokeo au unaona kidogo sana, usikate tamaa, wewe sio wa kwanza..

Lakini, mwishi wa siku utapungua tu.

Jipe kama miezi 3 uwe serious bila kuacha, UTASHANGAA!!

Pia..

Wingi wa sumu mwilini inaathiri afya ya mwili kiasi kwamba unakuwa tu unajisikia ovyo, uchovu uchovu, magonjwa yasiyoisha, kinga ya mwili inashuka.

Sumu zinaathiri ini na kulifanya lisifanye kazi kwa ufanisi. Mojawapo ya kazi ya ini ni kutengeneza protini ikiwemo homoni.

Kama ini halifanyi kazi sawasawa kwa sabau ya sumu, hata protini zinapungua na mfumo wa homoni pia unavurugika.

Hapo inaweza kupelekea mtu akapata kuongezeka uzito au akawa na kitambi na ikawa ni vigumu kupungua.

….”Utamsikia anasema, nimejaribu kila njia lakini sipungui”

Namna ya kuondoa sumu

Kitendo cha kuondoa sumu ni kitendo complex sana..

Asante Mungu kinafanyika bila sisi kujua.. inawezekana tungekuwa hatulali ili kusikilizia hizo harakati huko ndani.

Kuna aina mbili ya sumu..

Moja:

Ambazo zinayeyuka kwenye maji

Aina hizi ni rahisi sana kuzitoa mwilini kwa jasho au mkojo. Hapa ndio unaambiwa kunywa maji kuondoa sumu, ni aina hii.

Mbili:

Zinazoyeyuka kwenye mafuta.

Hapa tungesema tunywe mafuta mengi ili kuondoa hizi sumu.. lakini ole wako.. hahaha!

Ili kuondoa sumu zinazoyeyuka kwenye mafuta.. ini huwa linazibadilisha hizi kemikali ziwe katika hali ambayo zitaweza kuyeyuka kwenye maji ili zitolewe nje.

Kitendo hiki kinafanyika kila siku.. yaani ni muhimu kiwe kinafanyika kila siku ili sumu zisilundikane mwilini na kuleta madhara.

Namna hii ya kusaidia sumu kuondoka mwilini kila siku ndio ambacho tunakiita KUONDOA SUMU MILELE..

Kwa sababu hakuna hata siku moja utakuwa na sumu nyingi zilizozidi mwilini.

Ni tofauti na ile watu wengi wanayopenda kuifanya wanaiita detox..

Unakuta anakunywwa juisi za mbogamboga siku nzima au anakula matunda tu siku tatu nk.. zipo za aina nyingi.

Kwa sababu sumu zinaingia mwilini kila siku, huwezi kufanya hiyo program kila siku..

Hata hivyo..

Hizo program nazo ni nzuri japo ufanisi wake sio kwa 100% na sio ya kudumu.

Nimeibadilisha na kuiweka katika namna ambayo unaweza ukafanya kila siku bila kujisikia kuwa unafanya kitu special, kwahiyo utaweza kufanya kwa muda mrefu.

Chakula hai

Ukisikia chakula hai naona kabisa vile kachumbari inavyokuja haraka haraka kichwani..

Ni zaidi ya hapo…

Chakula hai; ni chakula ambacho kinatokana na mimea katika uasili wake.

Vyakula vinavyotokana na mimea, vina uwezo mkubwa wa kusaidia mwili kujisafisha.

Zaidi..

Vyakula hivi vina dawa ambazo zinasaidia kuondoa sumu mwilini.

Vyakula hivi ni kama matunda, mbogamboga na mbegu mbegu aina zote wkati huo punguza vyakula vinavyotokana na wanyama.

Pendelea tu kula vyakula vya asili vinavyotokana na mimea vinasaidia kuondoa sumu kila siku kidogo kidogo lakini kwa uhakika.

Wakati kula chakula hai ni nzuri kujenga afya ya mwili; kwenye suala la kuondoa sumu mwilini kuna kitu muhimu sana kinaitwa ..

…‘GLUTATHIONE’..

Hiki ni kirutubisho ambacho kina nguvu sana ya kuondoa sumu mwilini.

  • Kinasaidia kuondoa madini tembo ‘heavy metals’ hasa mercury wengine wanaiita zebaki.
  • kinaondoa mabaki ya dawa kama paracetamol
  • kinasafisha ini na kulinda ini lisiharibiwe.
  • Kinazima mioto
  • Hata kama una mafuta mengi kwenye ini au ini lina makovu, glutathione inasaidia ini lifanye kazi yake vizuri.
  • Hii inasaidia kubadilisha sumu zinazoyeyuka kwenye mafuta ziyeyuke kwenye maji ili zitolewe nje kirahisi.
  • Inasaidia pia usugu wa insulin na
  • inalinda afya ya mitochondrion kwahiyo inakusaidia kulinda a saratani.

Hizi kwa wingi unazipata kwenye mbogamboga kama jamii ya kabeji kama vile kabeji, brokoli, kauliflawa na kwenye  vitunguu maji na vitunguu saumu.

Vitu vingine vinavyoongeza wingi wa glutathione ni;

  • Curcumin kutoka kwenye bizari manjano
  • Melatonin; inapataikana kwa kupata infra-red light  inayopatikana kwenye mwanga wa jua.

Pia..

Mbogamboga za kijani kwa sababu ya wingi wa chlorophyll ‘ile ukijani wake’ zinasiaid apia kuondoa sumu mwilini..

Hizi jamii ya kabeji, kitunguu maji na kitunguu saumu.. fanya iwe sehemu ya milo yako kama unavyokulaga ugali kila siku.

Kula kabeji sio ushamba.. unaweza ukaila kama mboga au kwenye kachumbari au kwenye juisi. Vyovyote vile.

Kitunguu maji ukikikaanga kwenye mafuta unakiua kabisa.. inakuwa ni kama umemsulubisha mwokozi wako.

Ndio maana ujanja ni kukiweka kwenye kachumbari.. pendelea kula kachumbari mara kwa mara inakusaidia.

Kitunguu saumu, hata ukikipika kwenye chakula, ukaweka kwenye juisi, ukakinywa chenywe vyovyote vile kinakupatia faida zake.

Hivi ni vitu vya kawaida sana lakini ukivifanya kila siku vinakupa faida kubwa sana.

Kwahiyo..

Ukipunguza vyanzo vya sumu kama nilivyofundishakwenye somo lililopita halafu ukafanya hii ya chakula.. kwa sehemu kubwa unakuwa unafanikiwa.

Halaf ongeza na mazoezi ‘jasho linatoa sumu’ na kunywa maji ya kutosha. Ukisikia kiu kunywa maji sio soda baridi

..heshimu mwili wako..

PAMOJA NA  HAYO..

Kwenye EASY CHOPPER nimeweka ‘Glutathione’

Naamini wale waliotumia easy chopper ni mashahidi jinsi wanavyojisikia baada ya kutumia..

.. pamoja na kwamba inaongeza kasi ya mwili kuchoma mafuta na kukusaidia kupunguza uzito hata kama hufanyi mazoezi wala diet.. LAKINI

….. “Inaondoa sumu pia’’…

Kwahiyo..

Inasaidia pia ku-balance mfumo wa homoni

Mliokuwa na changamoto ya hedhi na wanaume mliokuwa na changamoto kwenye masuala yetu… hahaha..

…mmeona jinsi ilivyowasaidia  kwa sababu ukishaindoa sumu mambo mengi unaona yanakuwa kwenye mstari.

Mmoja akanambia .. “dr mbona toka nianze easy chopper choo kimeongezeka?’’

Ndio sehemu ya uchafu unaotoka..

Hata hivyo…

..Easy chopper sio ya kuharisha na wala sio chungu..

Pamoja na njia nilizokuelekeza hapo juu, unaweza kuongeza easy chopper ikakusaidia katika safari yako..

Inafaa sana hasa kwa wale ambao wapo katika mazingira magumu ya kupata chakula kizuri na wale wanaotaka matokeo ya haraka zaidi.

Kila mtu anaweza kuipata .. dozi ya mwezi 1 ni tshs. 50,000/- hapo unaweza ukapunguza kati ya kiko 2 hadi 10.

Nina mawakal kwenye baadhi ya mikoa, unaweza ukapata ukiwa mkoa wowote Tanzania na Kenya.

4 1 vote
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments
Share
Scroll to Top